Featured Poem:
Hatufundishwi Shuleni
Enlarge poem
Featured Poem:
Hatufundishwi Shuleni
Hutufundishwi Kujiamini/
Hatufundishwi Kujithamini/
Hatufundishwi Kujijua,
Kujitambua Sisi Ni Wakinanani/
Hatufundishwi Tukagundua
Wapi Tulikuwa Kabla Ya
Ukoloni/ Zaidi Ya Kuchukiana
Hatufundishwi Kupendana
Darasani/ Hata Sishangai
Nikisikia, Mwafrika Kuingia
Vitani Kisa Dini/
Hatufundishwi Faida ya
Kuungana/ Hatufundishwi
Umuhimu Wa Kushirikiana/
Kuweka Nguvu Pamoja
Biashara Zilete Maana/
Tunafundishwa Ukilema
Watu Wazima Kutegemeana/
“..Aliyeanguka Sio Wenu..”
Hatufundishwi Kuinuana/
Tunafundishwa Historia
Isiyoandikwa Na Sisi/
Historia Iliyobadilishwa
Historia Isiyonauhalisi/
Tunafundishwa Matatizo
Pasipo Njia Za Kuyatatua/
Inachosha, Yanazidi Ongezeka
Hakuna Linalopungua/
Hatufundishwi Tukajua Kuwa,
Waafrika Tuna maadui/
Kila Nyakati Twawindwa
Si Usiku Mchana Hata Asubui/
Mzungu Njama Nyingi
Katu Mapigo Hayapungui/
Tumechomwa Sumu Tumeachwa
Tunatizama Alama Ya Ndui/
Tunafundishwa Kuigiza Nyendo
Za Mzungu/ Tusichojua Hayomaigizo
Yanaongeza Ukungu/
Hutufundishwi Mifumo Ya Dunia/
Jinsi Gani Inafanya Kazi Ili
Tusije Angamia/ Waongozoji
Kitu Gani Haswa Walichokipania/
Agenda Zao Wapi Zilipolalia/
Hatufundishwi Uozo Wa “Umoja
Wa Mataifa” Nyuma Ya Pazia/
Hatufundishwi Kwanini Mashujaa
Wa Afrika Tunaendelea Kuwafukia/
Tunafundishwa Nadharia Bila Vitendo/
Tunafundishwa Subira, Eti Polepole
Ndio Mwendo/ Tunafundishwa Wagunduzi
Wa Afrika Tuliyoikaa Tokea Mwanzo/
Mambo Ya Vasco Dagama, Historia Ya Kitoto
Tufanye Ukatazo/
Hatufundishwi Jinsi Ya Kujilinda/
Hatufundishwi Jinsi Ya Kuyapinga
Mazito Yanayotushinda/
Hatufundishwi Kukwepa Propaganda
Kuondoka Kwenye Runinga/
Ili Twende Kusoma Tuondoe Ujinga/
Hatufundishwi Tukajijua Kiundani/
Ili Tuwe Imara Kimwili Na Akili
Yatupasa Tule Chakula Gani/
Hatufundishwi Elimu Ya Jinsia
Wengi Tunajifunzia Uwanjani/
Hatufundishwi Mahusiano,
Usione Ajabu Ni Malumbano
Nyumbani/
Hatufundishwi Kwanini Hakuna
Ajira Nchini/ Tunafundishwa Ajira
Zipo Tunasoma Kwa Matumaini/
Hatufundishwi Kujiajiri, Tumalize
Tuishi Kimasikini/ Hatufundishwi
Kujenga Bila Hofu Ya Kuanguka Chini/
70% Ya Vijana Wapo Vijiweni
Baada Ya Kuitimu Vyuoni/
Inabidi Iwe Hivyo Maana
Hatufundishi Kipi Kipo Mtaani/
Hatufundishwi Kwanini Sisi
Ni Masikini/ Masikini Wa Hali Ya
Chini Maisha Yetu Duni/
Kipi Chashusha Kabisa Hali
Yetu Ya Uchumi/ Mbona
Tunawanyama Tele Mbugani..?/
Mafuta Na Madini Yanachimbwa Ardhini…?/
Lakini Hatufundishwi, Kuuliza Kwanini..?/
Hatufundishwi Kuijenga Afrika/
Hatufundishwi Afrika “Mpya”
Nini Inataka / Hatufundishwi
Kuichukia Misingi Iliyotuzika/
Misingi Waliyoijenga
Ili Unyonyaji Usijekatika/
Kiukweli Tunafundishwa Kulala,
Katu Hatufundishwi Kuamka/
Hatufundishwi Kuijua Siasa/
Siasa Inaendeshwa Vipi Ndani
Ya Ulimwengu Wa Sasa/
Tunachofundishwa Ni Akili
Kuzipumbaza/ Hatufundishwi
Kwa Macho Matatu Dunia Kuiangaza/
Kuangaza Marekani Na China Wanavyotuburuza/
Tunahitaji Elimu Yenye Kuiakisi Afrika/
Itakayotuhusu Sisi Na Mazingira
Yanayotuzunguka/ Itakayorekebisha Makosa
Ya Wapi Tulipoanguka/ Itakayotuonyesha Njia
Na Vipi Tutainuka/ Itakayoturudisha Kwenye
Asili Mpaka Tutapojikumbuka/
Elimu Hii Ya Sasa, Elimu Hii Nimeichoka/
Tunahitaji Tufundishwe Historia Yetu/
Tunahitaji Tufundishwe Tamaduni Zetu/
Tunahitaji Tufundishwe Thamani Na Ushujaa
Wetu/ Tunahitaji Tufundishwe Wapi Walipoishia
Babu Zetu/ Ili Juhudi Zao Ziendelezwe Visibezwe
Vizazi Vyetu/ Tunahitaji Tufundishwe Juu Ya Imani
Na Dini Zetu/
Tunahitaji Tufundishwe Kutofautisha
Kati Ya Taarifa na maarifa/
Ili Tusioshwe Ubongo, Uongo Uongo
Usilete Nyufa/
Tunahitaji Tufundishwe Chanzo
Cha Magonjwa Kama Ebola Ona
waafrika Wanavyokufa/
Tunahitaji Tufundishwe Kujiongoza
Tuondoke Utumwani/
Tuhitaji Tufundishwe Ili Tusirudishwe
Mashambani/
Tunahitaji Tufundishwe, Vipi Izalishwe
Isisafirishwe Katani/
Tunahitaji Tufundishwe Kupendana
Waafrika/ Chuki Yatutafuna, Umoja
Hatuna Twaingilika/
Tunahitaji Tufundishwe Manufaa
Ya Elimu Tuipatayo/
Elimu Tuipatayo Ituondoshe
Kwenye Hali Tulionayo/
Elimu Tuipatayo, Ikamilishe Safari
Tuijengayo/
Elimu Tuipatayo Ilishe Wengi
Isiache Wengine Wapige Mwayo/
Tunahitaji Tufundishwe Wizi
wa Warumi Na Wagiriki/
Kubeba Kila Kilichochetu Kusema
Chao Wakadiriki/
Dini, Sanaa, Sayansi, Uandishi,
Vyote Tulianzisha Sisi Hawatuandiki/
Tunafundishwa Uongo, Lakini, Ukweli
Haubadiliki/
Tunahitaji Tufundishwe Haki
Zetu Za Msingi/
Ili Uonevu Uondoshwe Maana
Manyanyaso Ya Polisi Ni Mengi/
Malcolm X Alisema,
“Hakuna Mtawala Anayemfundisha
Mtumwa Kuwa Huru”
Basi Tufundishane Kuikata Minyororo
Ikiwa Kweli Tunauhitaji Uhuru/
Translation:
“Hatufundishwi Shuleni” means “What They Don’t Teach Us in School”. In this poem Justin shares his concerns about the Tanzanian education system. He believes it is designed to keep black people weak and meek, and people should continue sending their children through this system if they do not want them to be strong, independent, and powerful people. The poet says they are not taught about self-confidence, self-valuing, self-education (knowledge of self), health, nutrition, relationships, sex and sexuality. They are not taught how to question and to reason. Justin is advocating for a new education system, one that will instil a sense of pride, teach them about their true history, and redefine the brains of many brainwashed Africans. The education system needs to build a strong people.
Hutufundishwi Kujiamini/
Hatufundishwi Kujithamini/
Hatufundishwi Kujijua,
Kujitambua Sisi Ni Wakinanani/
Hatufundishwi Tukagundua
Wapi Tulikuwa Kabla Ya
Ukoloni/ Zaidi Ya Kuchukiana
Hatufundishwi Kupendana
Darasani/ Hata Sishangai
Nikisikia, Mwafrika Kuingia
Vitani Kisa Dini/
Hatufundishwi Faida ya
Kuungana/ Hatufundishwi
Umuhimu Wa Kushirikiana/
Kuweka Nguvu Pamoja
Biashara Zilete Maana/
Tunafundishwa Ukilema
Watu Wazima Kutegemeana/
“..Aliyeanguka Sio Wenu..”
Hatufundishwi Kuinuana/
Tunafundishwa Historia
Isiyoandikwa Na Sisi/
Historia Iliyobadilishwa
Historia Isiyonauhalisi/
Tunafundishwa Matatizo
Pasipo Njia Za Kuyatatua/
Inachosha, Yanazidi Ongezeka
Hakuna Linalopungua/
Hatufundishwi Tukajua Kuwa,
Waafrika Tuna maadui/
Kila Nyakati Twawindwa
Si Usiku Mchana Hata Asubui/
Mzungu Njama Nyingi
Katu Mapigo Hayapungui/
Tumechomwa Sumu Tumeachwa
Tunatizama Alama Ya Ndui/
Tunafundishwa Kuigiza Nyendo
Za Mzungu/ Tusichojua Hayomaigizo
Yanaongeza Ukungu/
Hutufundishwi Mifumo Ya Dunia/
Jinsi Gani Inafanya Kazi Ili
Tusije Angamia/ Waongozoji
Kitu Gani Haswa Walichokipania/
Agenda Zao Wapi Zilipolalia/
Hatufundishwi Uozo Wa “Umoja
Wa Mataifa” Nyuma Ya Pazia/
Hatufundishwi Kwanini Mashujaa
Wa Afrika Tunaendelea Kuwafukia/
Tunafundishwa Nadharia Bila Vitendo/
Tunafundishwa Subira, Eti Polepole
Ndio Mwendo/ Tunafundishwa Wagunduzi
Wa Afrika Tuliyoikaa Tokea Mwanzo/
Mambo Ya Vasco Dagama, Historia Ya Kitoto
Tufanye Ukatazo/
Hatufundishwi Jinsi Ya Kujilinda/
Hatufundishwi Jinsi Ya Kuyapinga
Mazito Yanayotushinda/
Hatufundishwi Kukwepa Propaganda
Kuondoka Kwenye Runinga/
Ili Twende Kusoma Tuondoe Ujinga/
Hatufundishwi Tukajijua Kiundani/
Ili Tuwe Imara Kimwili Na Akili
Yatupasa Tule Chakula Gani/
Hatufundishwi Elimu Ya Jinsia
Wengi Tunajifunzia Uwanjani/
Hatufundishwi Mahusiano,
Usione Ajabu Ni Malumbano
Nyumbani/
Hatufundishwi Kwanini Hakuna
Ajira Nchini/ Tunafundishwa Ajira
Zipo Tunasoma Kwa Matumaini/
Hatufundishwi Kujiajiri, Tumalize
Tuishi Kimasikini/ Hatufundishwi
Kujenga Bila Hofu Ya Kuanguka Chini/
70% Ya Vijana Wapo Vijiweni
Baada Ya Kuitimu Vyuoni/
Inabidi Iwe Hivyo Maana
Hatufundishi Kipi Kipo Mtaani/
Hatufundishwi Kwanini Sisi
Ni Masikini/ Masikini Wa Hali Ya
Chini Maisha Yetu Duni/
Kipi Chashusha Kabisa Hali
Yetu Ya Uchumi/ Mbona
Tunawanyama Tele Mbugani..?/
Mafuta Na Madini Yanachimbwa Ardhini…?/
Lakini Hatufundishwi, Kuuliza Kwanini..?/
Hatufundishwi Kuijenga Afrika/
Hatufundishwi Afrika “Mpya”
Nini Inataka / Hatufundishwi
Kuichukia Misingi Iliyotuzika/
Misingi Waliyoijenga
Ili Unyonyaji Usijekatika/
Kiukweli Tunafundishwa Kulala,
Katu Hatufundishwi Kuamka/
Hatufundishwi Kuijua Siasa/
Siasa Inaendeshwa Vipi Ndani
Ya Ulimwengu Wa Sasa/
Tunachofundishwa Ni Akili
Kuzipumbaza/ Hatufundishwi
Kwa Macho Matatu Dunia Kuiangaza/
Kuangaza Marekani Na China Wanavyotuburuza/
Tunahitaji Elimu Yenye Kuiakisi Afrika/
Itakayotuhusu Sisi Na Mazingira
Yanayotuzunguka/ Itakayorekebisha Makosa
Ya Wapi Tulipoanguka/ Itakayotuonyesha Njia
Na Vipi Tutainuka/ Itakayoturudisha Kwenye
Asili Mpaka Tutapojikumbuka/
Elimu Hii Ya Sasa, Elimu Hii Nimeichoka/
Tunahitaji Tufundishwe Historia Yetu/
Tunahitaji Tufundishwe Tamaduni Zetu/
Tunahitaji Tufundishwe Thamani Na Ushujaa
Wetu/ Tunahitaji Tufundishwe Wapi Walipoishia
Babu Zetu/ Ili Juhudi Zao Ziendelezwe Visibezwe
Vizazi Vyetu/ Tunahitaji Tufundishwe Juu Ya Imani
Na Dini Zetu/
Tunahitaji Tufundishwe Kutofautisha
Kati Ya Taarifa na maarifa/
Ili Tusioshwe Ubongo, Uongo Uongo
Usilete Nyufa/
Tunahitaji Tufundishwe Chanzo
Cha Magonjwa Kama Ebola Ona
waafrika Wanavyokufa/
Tunahitaji Tufundishwe Kujiongoza
Tuondoke Utumwani/
Tuhitaji Tufundishwe Ili Tusirudishwe
Mashambani/
Tunahitaji Tufundishwe, Vipi Izalishwe
Isisafirishwe Katani/
Tunahitaji Tufundishwe Kupendana
Waafrika/ Chuki Yatutafuna, Umoja
Hatuna Twaingilika/
Tunahitaji Tufundishwe Manufaa
Ya Elimu Tuipatayo/
Elimu Tuipatayo Ituondoshe
Kwenye Hali Tulionayo/
Elimu Tuipatayo, Ikamilishe Safari
Tuijengayo/
Elimu Tuipatayo Ilishe Wengi
Isiache Wengine Wapige Mwayo/
Tunahitaji Tufundishwe Wizi
wa Warumi Na Wagiriki/
Kubeba Kila Kilichochetu Kusema
Chao Wakadiriki/
Dini, Sanaa, Sayansi, Uandishi,
Vyote Tulianzisha Sisi Hawatuandiki/
Tunafundishwa Uongo, Lakini, Ukweli
Haubadiliki/
Tunahitaji Tufundishwe Haki
Zetu Za Msingi/
Ili Uonevu Uondoshwe Maana
Manyanyaso Ya Polisi Ni Mengi/
Malcolm X Alisema,
“Hakuna Mtawala Anayemfundisha
Mtumwa Kuwa Huru”
Basi Tufundishane Kuikata Minyororo
Ikiwa Kweli Tunauhitaji Uhuru/
Translation:
“Hatufundishwi Shuleni” means “What They Don’t Teach Us in School”. In this poem Justin shares his concerns about the Tanzanian education system. He believes it is designed to keep black people weak and meek, and people should continue sending their children through this system if they do not want them to be strong, independent, and powerful people. The poet says they are not taught about self-confidence, self-valuing, self-education (knowledge of self), health, nutrition, relationships, sex and sexuality. They are not taught how to question and to reason. Justin is advocating for a new education system, one that will instil a sense of pride, teach them about their true history, and redefine the brains of many brainwashed Africans. The education system needs to build a strong people.
All work on this website is licensed under a Creative Commons Attribution-NonCommercial-ShareAlike 2.5 South Africa License.
I’m so proud of you my fellow poet brother….teach the world through poetry.
its nice poetic work i ever attended alot of poetry event also yours is among of the best…keep it up comrade
Brother GSP shows a clear picture of what we think we are but we are not and he is trying to tell us about the real picture about African spirit and who we got to be . He wants black folk to live and believe in African values
Hakika mara ya kwanza kukusikiliza nilipata faraja isiyo kifani. Uandishi wako wanihamasisha kimatendo. Hongera sana.
one of my favorite poet,your poems reflect the reality of what africans should do..bless
Bro ur poety brighten my morning, deep knowledge, thank you coz we dwell in da same circle
Thnx Kakoko,, Am proud ov yu Bro,, keep it up
Hatufundishwi kushukuru..
Wooow speechless braa keep it up we all on the same mission @lbtanzania
Truth brother…As always